Mimea tiba kupitia mimea ya majumbani


Mimea tiba kupitia mimea ya majumbani


  • Thread starter




Mmea ni majabu ya Mungu kwetu .

Mmea hapo kwenye picha :

๐ŸฅฌKisukuma unaitwa Mjorwambogo.
๐ŸฅฌKikamba unaitwa Ithaa.
๐ŸฅฌKikikuyu unaitwa Mwino au mwinu.
๐ŸฅฌKijaruo unaitwa Ovino au owinu.
๐ŸฅฌKimeru unaitwa Kirao au Murao.
๐ŸฅฌKitaita unaitwa Mbinu au Mshua.
๐ŸฅฌKiiraq unaitwa Nkharerei.
๐ŸฅฌKihehe huitwa Mulimuli.
๐ŸฅฌKisambaa huitwa Mzangazi.

Kuhusu matibabu :

๐Ÿฅฌ Huo mti hutibu magonjwa ya ini...
๐ŸฅฌHutibu vidonda vya tumbo. Hutibu malaria, typhoid na ameba.
๐ŸฅฌHutibu kisonono. Huondoa sumu zote mwilini na kupunguza mafuta.
๐ŸฅฌMtidawa huu hushusha shinikizo la damu yaani presha ya kupanda.
๐ŸฅฌHutibu chlamydia. Hutibu magonjwa ya mifupa. Magonjwa yote ya mfumo wa uzazi wa mwanamke hutibiwa na mti huu...
๐ŸฅฌMti huu humwezesha mwanamke kushika ujauzito ikiwa hajakoma hedhi.Hii hufanyika kwa kuondoa uvimbe wowote kwenye mfumo wa uzazi, ini, bandama, figo, kusafisha kizazi, kurutubisha mayai na kuongeza uwezekano wa kupata ujauzito

๐Ÿฅฌ Mti huu hurudisha mzunguko wa hedhi na kuuweka uwe sawa ikiwemo kuondoa maumivu kipindi cha hedhi...
๐ŸฅฌMti huu huondoa uvimbe wa aina yoyote ndani ya mirija ya uzazi, ovari, uterus au kizazi kwa muda wa wiki tatu tuu..

NAMNA YA KUTENGENEZA

๐ŸฅฌChukua majani yake. Hakikisha huchanganyi na mbegu zake. Chukua majani tuu. Chukua mengi kadri uwezavyo. Yaanike mahali safi ndani, Yasambaze kabisa. Baada ya siku tatu kama mahali hapo pana joto la kutosha (hapo ndani na siyo nje kwenye jua) yatakauka.Saga ili kupata unga laini, Waweza kusaga hata kwa kufikicha tuu kwa mkono. Ni malaini na yanasagika kwa haraka mno ikiwa yamekauka vizuri. Waweza kusaga kwa kutumia brenda pia...

NAMNA YA KUTUMIA

๐Ÿฅฌ Isipokuwa ugonjwa wa kisonono, tumia kijiko kidogo ndani ya maji ya moto nusu kikombe cha chai asubuhi na jioni kwa muda wa week mbili. Baada ya hapo, nenda ukapime hutaona kitu.

๐ŸซKumbuka: Mtidawa huu utakufanya uharishe kama mara tatu kila unapokunywa. Kadri tatizo linavyoendelea kuisha mwilini, kuharisha nako kunapungua na mwisho kupotea kabisa. Wagonjwa1738690671023.jpg

NDURA 1738690929361.jpg

Haya Ni Matunda ya Ndula wengine huita Ndulele , Wengila Ntula Ntula, Kwa wasukuma wanaita Mantindira ...

Maarufu sana kwa wale wanaosumbuliwa na Meno ...

Na Yapo Ya Aina Mbili , Moja huwa upo unakuwa haukui sana kuelekea Juu , na mwingine huwa unarefuka sana kwenda juu...

Sasa Haya ni Yale yanayolefuka sana ..

JE Upande wako uliwahi kuyatumia kujitibu nini ?

Utashare kwenye comment hapo chini.

Mimi Huwa nautumia kutibu Mtu anayesumbuliwa na kifua either kinabana kwa mda huo , au Kinauma ...

Cha kufanya Chukua matunda yake kadhaa matatu hadi 8 kisha kata Katikati kila tunda , Chemsha ktk maji ya Nusu lita , kwa dk 10 ,Baada ya hapo ...

Kwa Mtu Mwenye miaka 10 -18 atumie Nusu ya kisoda (mfuniko wa chupa ya soda) mara mbili kwa siku

Kwa Mtu mwenye miaka 18 na kuendelea atumie kisoda kimoja mara mbili kwa siku ...

Usizidishe hapo , Huwa ni Dawa kali sana hiyo

Matumizi siku 5 hadi 7

Lakini pia kwa Mama Mjamzito , Ambaye anatarajia kwenda kujifungua , Au Anatarajia kujifungua , Chimba Mizizi yake , Tafuna ... baada ya dk 10 , Utajifungua hata bila Msaidizi

Kwa wanaume waliooa , kama unataka kuboost Chimba mizizi yake , Unaweza ukatafuna na karanga au unaichemsha kwa dk 15 baada ya hapo kunywa kikombe kimoja , then tafuna karanga punje kama 20 ,au kula Ndizi mbivu mbili .. itakusaidia ..

Kama dawa ya fangasi

1. Chukua matunda matatu (usimenye, wala usitoe mbevu)
2. Katakata vipande vidogo sana
3. Chukua mafuta ya nazi vijiko 2 vya mezani
4. Blend mchanganyiko huu uwe laini kabisa (uji)
5. Paka eneo lenye fangasi asubuhi na jioni, kwa siku 7-10

Angalizo: usipake kwenye fangasi za sehemu za siri, inawasha sana

MAJANI YAKE

Mwenye kisukari chukuwa majani yake ponda ponda upate unga wake utatumia kunywa kwenye maji ya vuguvugu kutwa mara tatu Kwa siku 14 nenda kapime Leta mrejesho..

๐Ÿ”ฅ Kwa mtu anayesumbuliwa na tumbo la hedhi upate unga wa majani tumia kwenye maji moto ni tiba nzuri pia

Lakini pia kwa wanaoumwa meno, kama jino limetoboka chukua mzizi wa mti wa ndura mkavu chemsha na chumvi kisha nyunyuzia kwenye shimo. Kama halijatoboka sukutua Mara tatu kwa siku...

Pia matunda yake hutumika kutolea funza , mdomoni ambao ndio husababisha meno kuuma au kutoboka..

๐Ÿ”ฅ Kwa watoto wadogo wa kiume wenye ugonjwa wa ngiri kende kusinyaa. Chukua mizizi ya mti huu changanya na mzizi wa mpapai dume itimie saba Chemsha mpe anywe kutwa Mara mbl kwa ck saba

๐Ÿ”ฅTiba Ya Chango Kwa Wanawake Na Wanaume...

Andaa unga wa mizizi ya mkunde pori na ndura (ndulele) vyote katika kiwango cha vijiko 15, andaa maji moto robo lita kisha weka robo kijiko ya mchanganyiko kunywa kutwa mara mbili kwa wiki nne..

Kama Unasumbuliwa na Figo au Ini

Chemsha mizizi ya ndulele, msikesike(lufyambo), majani ya mstafeli, majani ya mpera, mizizi ya mtopetope, kitunguu swaumu chemsha kwa pamoja na mafuta ya HABATI SAUDA Kisha baada ya hapo utachukua nusu kikombe cha hiyo dawa yako utatia kijiko cha dawa ya HABATI SAUDA ya unga kisha utakunywa fanya zoezi hilo kutwa mara 3 ndani ya siku 21- 40
  • Thread starter
  • #3
Mti wa mlingoti (au Maste tree) au muashoki huponya:

๐ŸŒฟMalaria
๐ŸŒฟHoma ya matumbo
๐ŸŒฟCandidiasis
๐ŸŒฟArthritis
๐ŸŒฟVidonda vya tumbo
๐ŸŒฟShinikizo la damu
๐ŸŒฟKisukari
๐ŸŒฟKuharibika kwa ini
๐ŸŒฟKushambuliwa na minyoo wa matumbo.

Maandalizi:

Chemsha maji yenye vijiko 3 vya unga wa majani yaliyokaushwa kwa muda wa dakika 10. Kunywa kikombe cha chai mara mbili kwa siku. (Boil 3 tablespoons of the dried powdered leaves for 10mins. Drink a teacup twice daily. )

As1738691002048.jpgili huponya
  • Thread starter
  • #4
MSTAFELI NA UGONJWA WA UKOMA PAMOJA NA SARATANI MBALIMBALI
1738691036886.jpg

Juisi ya tunda la mti huu hutumika kutibu
Ukoma (leprosy).

Majani haya ya mstafeli yamethibitika siyo kutibu
saratani au kansa ya tezi dume bali na aina
nyingine za saratani zaidi ya 12 ambazo ni
pamoja na:

1. Saratani ya damu
2. Saratani ya matiti
3. Saratani ya mlango wa kizazi
4. Saratani ya mapafu
5. Saratani ya ini
6. Saratani ya mdomo
7. Saratani ya kwenye ulimi
8. Saratani ya kongosho
9. Saratani ya kwenye mji wa uzazi
10. Na sratani nyingine nyingi.

Majani ya mstafeli ni dawa nzuri dhidi ya bakteria na fangasi mbalimbali mwilini na hivyo ni kinga dhidi ya maambukizi ya kila namna.
Majani ya mstafeli yanatibu pia:

1. Kisukari
2. Gout (maumivu ya jongo)
3. Maumivu ya mgongo
4. Yanaongeza kinga ya mwili
5. Yanaimarisha afya ya tumbo kwa ujumla
6. Kufunga choo
7. Msongo wa mawazo (stress)
8. Yanaimarisha afya ya nywele
9. Yanaimarisha afya kwenye mfumo wa upumuwaji
10. Yanaongeza afya ya ngozi
11. Mazuri kwa afya ya moyo
12. Yanadhibiti homa na kutuliza joto la mwili
13. Dawa nzuri kwa matatizo mengi ya uzazi
14. Huongeza stamina ya mwili na kurahisisha kupona haraka unapokuwa mgonjwa
15. Hutibu jipu na vivimbe
16. Hudhibiti ukuwaji wa bakteria, virusi, vijidudu nyemelezi na uvimbe
17. Ni tiba ya asili ya maumivu ya mishipa, yasage majani yake mpaka yalainike kabisa kisha paka taratibu eneo la mshipa lililo na maumivu mara 2 kwa siku

Dawa kubwa ya saratani ambayo watu wengi hawaifahamu …

Kuna wakati namtafakari Mungu na nashindwa kupata majibu kwamba kuna wakati watu wanateseka sana lakini bila sababu yoyote maalumu zaidi ya kukosa tu maarifa Kile nitakushangaza kidogo hapa ni kuwa uwezo huu wa majani ya mstafeli kutibu kansa uligundulika tangu mwaka 1976 na taasisi ya saratani ya Marekani lakini matokeo yake hayajawahi kuwekwa hadharani kwa watu!

Kwanini hawakutaka kutangaza kwa watu?
Hakuna mtu anayejuwa kwa hakika sababu ni nini iliyowafanya wabaki na matokeo
  • Thread starter
  • #6
Kitaalamu mmea huu unaitwa Kalanchoe Marmodata Baker ,jina mama ni Kalanchoe ambapo aina zingine ni kama Kalanchoe prittwitzii Kalanchoe Pinnata Kalanchoe Densiflora Rolfe na Kalanchoe Crenata , Je kwenu unaufahamu kwa jina lipi ??

Huu mmea una maajabu yake!

■■ Kwa wanawake husaidia kusafisha mirija (kwa wenye maambukizi ya bakteria au fangasi) kwenye mirija ya uzazi na U.T.I sugu isiyotibika kwa Azuma wala sindano

■■ Hutumika pia kwa watoto wenye shida ya kupumua,

■■ Kwa wenye maumivu makali ya madonda ya tumbo hutumia kutuliza maumivu

Unachukua majani kadhaa kisha unayababua kwenye joto kisha unafikicha na kukamua, yana maji mengi, ukifikisha nusu glass ongeza maji ya kawaida (Ya Uvuguvugu) mpaka ijae kisha kunywa asubuhi na usiku pia utafanya hivyo angalau kwa siku 4 hadi 7

Maji yake hayana harufu mbaya wala hayachefui.

Siyo hivyo tu !

Kama mtoto wako mchanga alikunywa maji machafu akawa anakoroma basi hii ni dawa iinsaidia kusafisha!! Unaibabua kwenye Moto unamwekea Kila pua tone moja na mdomoni moja baada ya muda kidogo anapiga chafya uchafu unatoka hata akicheua anakuwa anatoa malenda lenda atakuwa sawa.

Kwa Miguu inayouma unyababua majani kwenye moto kisha1738691125048.jpg unachua.

Kwa wanaoumwa MASIKIO, ukibabua majani hayo kwa moto, ukaweka matone mawili au matatu kwenye sikio linaloumwa asubuhi na jioni kila siku unapona ndani ya siku 3 hadi 5
  • Thread starter
  • #8
Chai ya unga wa Tangawizi + mdalasini + Manjano / tumeric(Binzari) mchanganyo huo hutibu:

๐ŸŒฟKumwaga manii kabla ya wakati
๐ŸŒฟKikohozi na baridi(Pneumonia)
๐ŸŒฟPumu
๐ŸŒฟMawe kwenye figo
๐ŸŒฟMfadhaiko
๐ŸŒฟKichefuchefu
๐ŸŒฟOsteoarthritis
๐ŸŒฟMsongo wa mawazo
๐ŸŒฟMaumivu ya hedhi

Weka kijiko kimoja cha kila mchanganyo hapo juu ndani ya maji ya moto na kunywa kabla ya kula kitu chochote asubuhi ..

As1738691201804.jpgili huponya.
  • Thread starter
  • #9
FAIDA ZA LIMAO /KUNYWA MAJI YA LIMAO , NI NYINGI SANA NARUDIA KWA FAIDA YA WAGENI JAPO SITAZISEMA ZOTE ...

Lemon juice + water
Juisi ya limao na maji

KILA ASUBUHI HAKIKISHA KABLA KUFANYA CHOCHOTE UNAKUNYWA KINYWAJI HIKI

Hapo kuna malimao mawili ndani ya glasi ya maji .

Hiki ni kinywaji sahihi kuanza nacho Kila siku

Ukijenga tabia ya kunywa juisi hii utaona maajabu makubwa sana kwenye afya yako.ndani tu ya siku 30 ...

1.Huimarisha kinga ya mwili Kwa kuwa lina vitamin C

2.Husafisha utumbo mpana, huzuia constipation-Dietary Fiber

3.Hutibu malaria, kipindupindu, ni Antibacteria

4.Huweka sawa pH ya damu-Limao hufanya damu iwe alkaline, Kuongeza Damu Mwilini ..

5.Husaidia mmeng'enyo wa chakula-Husaidia/huchochea kuzalishwa kwa nyongo

6.Huzuia magonjwa ya moyo na presha ya juu ya damu-pH balance calcium, magnesium na potassium

7.Hutibu homa na mafua

8.Huondoa sumu mwilini-alkaline blood/pH balance

9.Hutibu arthritis na Rheumatism-Husafisha damu na huondoa uric acid

10.Huondoa mikunjo kwenye ngozi

11.Huondoa maumivu ya kuumwa na nyuki

12.Huboresha afya ya macho

13.Huzuia kuvuja kwa damu ndani ya mwili au puani

14.Huondoa makovu kwenye ngozi

15.Kisukari(Type 1 diabetes) hasa kwa watoto kwa heri

16.Cancer ya utumbo mpana kwa heri

17.Cancer yoyote kwa heri kama utakuwa na tabia ya kunywa maji ya limao

18.Kipindupindu kwa heri kama una tabia ya kunywa maji ya limao kila asubuhi

19.Soko la dawa za malaria litashuka kama watu watakuwa wanatumia maji ya limao

20.Kwa watu wenye maumivu ya magoti huweza kupata nafuu kwa kunywa maji ya limao tu na kusahau dawa za hospitalini.

21.Kwa kina dada warembo kwa kutumia limao tu wataepukana na vipodozi vyenye sumu kama Oxybenzone,Avobenzone

Escamule , Octocryclene Zinazosababisha kansa ili kungarisha ngozi zao..

Yaani usiende mbali sana, chukulia cancer, kisukari na malaria pekee....

Kama watu watapenda kutumia maji ya limao mara kwa mara kwenye maisha yao ina maana soko la dawa za cancer, kisukari na
  • Thread starter
  • #11
KWA MALARIA SUGU NA YA KAWAIDA

Tafuta Majani ya mpapai twanga au saga upate juice , Ichuje kisha chukua vijiko vitatu weka kwenye maji glas moja , kunywa mara tatu kwa siku tatu , Leta Ushuhuda hapa.

Juice ya mpapai , Ni tiba ya haraka zaidi kwa malaria ndani ya siku tatu malaria inakuwa hadi1738691301673.jpgthi
  • Thread starter
  • #14
Ukiwa na huu mmea huo kwenye picha ujue una dawa ya kikohozi na UTi kwa wakati mmoja!

■■ Wengine huita Kibwelabwezi
■■ wengine Mlavumba

●● Ukiwa na kikohozi sugu
Chuma hayo majani, tafuna na kipande cha muwa ili kupunguza makali/uchungu wa hiyo dawa

Ukitafuna unahisi hadi masikio yanapika kelele za shangwe

●● Kwa magonjwa ya mfumo wa mkojo kama UTI, Chango , kisonono, uvimbe kwenye mfumo wa mkojo
Pika chai ya haya majani

Kunywa mara 3 kutwa

●● Kuongeza Nguvu za Kiume
Tafuna jani 1 kila siku kwa siku 14

●● Pia Ni Tiba kwa Presha ya kupanda ..

●●Na ni Tiba ya Malaria, Matumizi yake chemsha kunywa Mara tatu

Note: kwa Mtu mwenye pressure ya ku1738691395079.jpgshuka asitumie hii
  • Thread starter
  • #17
Sida Acuta

Mmea huu ni mgumu sana kung'oa nadhani wengi tunaujua au tumeshawahi kuuona.sijui kilugha wala kiswahili chake.

Huu mmea

*Chai ya mizizi yake inaongeza nguvu za kiume

*Ukiponda majani yake kwa kuchanganya na kitungu swaumu ni dawa ya jipu

*Chai ya majani yake inasaidia mwanamke kujifungua haraka bila maumivu makali sana

*Chai ya mmea huu ni nzuri kwa mwanamke ambaye uzazi umegoma. Kunywa hii kwa siku 5 kuanzia unapoona damu ya hedhi
Mungu atajaalia

Je umeutambua mmea huu? Unajua niini kuhusu huu mmea kwa zaidi ya ni1738691559162.jpgliyoyaelezaa??

Comments

Popular posts from this blog

Madhabahu ni nini?

Kifungo cha utumwa

KIFO CHA MAPEMA: UFUNUO WA KIROHO